Post by Yona Maro on Dec 11, 2005 6:30:25 GMT -5
Katika ulimwengu huu unaokabiliwa na matatizo mengi ya kiafya, yapo maradhi hatari yaliyosahaulika--kiharusi (Stroke). Kutokana na hatari yake, wanatiba wameutaja ugonjwa huo kama 'Mshtuko wa Akili.' Lakini ni kwa nini kiharusi kinatokea? Sayansi na teknolojia imefanya na kugundua nini kuhusiana na ugonjwa huo? Je, wanyama wengine--tofauti na mwanadamu--wanapatwa na ugonjwa huo? Kuna kinga yoyote? Anaandika WILLIAM SHAO.
KIHARUSI au, kama wanasayansi wengine wanavyoutaja, 'mshtuko wa akili', ndiyo sababu kubwa ya vifo na ulemavu wa kudumu kwa watu katika nchi nyingi. Maneno yenyewe, yaani "mshtuko wa akili" (stroke--au kiharusi) yanaelezea hali ya ghafla ambayo "kushambuliwa kwa ubongo" hutokea.
Dakika moja, unaweza kujihisi vizuri, kitambo kidogo baadaye, unahisi kama vile umeshtuliwa na umeme au radi na kukuacha umelemaa--hivyo ndivyo kiharusi kinavyoweza kugeuza maisha yako kwa ghafla na kwa njia ya kushtua sana. Dakika moja unaweza kuwa mzima wa afya njema, dakika chache baadaye unagundua kuwa baadhi ya viungo vya mwili wako--mguu, mkono au mdomo--havifanyi kazi.
Ugonjwa huo ukiisha kukulemaza na kukudhoofisha kabisa, unaweza kukufanya ushindwe kuongea, ukiharibu kabisa hisia zako, ukibadili utu wako na uwezo wako wa kutambua mambo. Akili yako na uwezo wako wa kufikiri huharibika. Unaweza kushindwa kumtambua mkeo, mumeo, mwanao, nduguyo au mzazi uliyemzoea sana.
Kitabu All You Need To Know About Stroke kinasimulia kuhusu yaliyompata Alan Smith. Kinasema: "Siku ya Jumatano, alikuwa na umri wa miaka 54 akiwa katika hali yake ya kawaida na mwenye afya nzuri. Alhamisi (siku moja baadaye), alipokuwa na mkewe wakinunua vitu dukani, ghafla Smith alipoteza uwezo wake wa kuongea, na uso wake ukaumbuka. Mwili wake ulidhoofika, na alipepesuka, kama kwamba alikuwa amelewa." Kwanini? Kwa sababu "...Smith alikumbwa na kiharusi."
Baada ya kiharusi hicho, Smith alilemaa sana kiasi cha kushindwa kufanya mambo rahisi kufanywa--kama vile kuoga, kuvaa nguo na kula. Alishindwa kuandika, kusoma, kuchana nywele zake na kusalimiana na yeyote kwa kumpa mkono. Alikumbwa na vipindi vya kutokwa machozi ambayo hakutaka yatoke lakini hakuweza kuyazuia. Alikuwa akitokwa na mkojo asioweza kuuzuia pamoja na uchovu uliomzidi nguvu. Heshima yake ilivunjika.
Katika mambo yote hayo, uwezo wa kufikiri wa Smith haukuharibika, lakini wakati mwingine aliona aibu alipohisi kwamba labda wengine walimwona kama punguani. Ilimchukua muda mrefu kabla hajaweza kuongea tena, na alipoweza kufanya hivyo, alisema: "...Karibu nilihisi kwamba huo ulikuwa mwisho wa maisha yangu."
Kiharusi kinaweza kumpata mtu yeyote. Kitaalam, ubongo (wa mwanadamu) ndicho kiungo cha mwili kinachoweza kuharibika kwa urahisi sana, pengine kuliko kiungo kingine chochote, na huenda hicho ndicho kiungo cha maana zaidi kwa mwili wa mwanadamu kwa kuwa kinaongoza sehemu nyingine zote za mwili kikiagiza mkono, mguu, jicho au mdomo ufanye nini.
Kwa mujibu wa wanasayansi, ubongo wa binadamu, ukiwa na asilimia 2 tu ya uzani wote wa mwili wake, una chembe za neva zaidi ya bilioni kumi, ambazo huwasiliana daima ili kuzalisha fikra, mwendo na hisia.
Ubongo pia hutegemea hewa ya oksijeni. Ikiwa ubongo utanyimwa hewa hiyo, hata kama ni kwa sekunde chache tu, nyuroni zinazoweza kuharibika kwa urahisi hudhoofika haraka na kwa urahisi zaidi. Hilo likiendelea kwa zaidi ya dakika moja, madhara ya ubongo hutokea na kisha kuwa makubwa zaidi.
Hali hii huitwa ischemia, ukosefu wa oksijeni, hasa unaosababishwa na kuziba kwa arteri (moja ya mrija minene inayotoa damu kutoka moyoni na kupeleka sehemu nyingine za mwili). Ikiwa hali hiyo itaendelea kwa muda sekunde chache kiasi, matokeo ya mwisho yanakuwa ni mshtuko wa akili, au kiharusi (stroke).
Utaalam unaonyesha kuwa kila kiharusi ni tofauti na kinaweza kuwaathiri watu tofauti kwa njia tofauti. Ingawa hakuna yeyote anayepatwa na kila tokeo linalowezekana la kiharusi, matokeo yanaweza kutofautiana kuanzia madogo yasiyoonekana wazi hadi makubwa yanayoonekana wazi kwa njia ya maumivu. Sehemu ya ubongo inayopatwa na kiharusi huamua ni sehemu gani ya mwili itakayodhoofika.
Tatizo la kawaida linalosababishwa na kiharusi ni udhaifu wa kupooza miguu au mikono. Kwa kawaida, huo huwa ni upande mmoja tu wa mwili--upande ulio kinyume cha upande wa ubongo ambako kiharusi kimetokea.
Hivyo madhara ya ubongo wa upande wa kulia husababisha mwili kupooza upande wa kushoto, na madhara ya ubongo wa upande wa kushoto husababisha mwili kupooza upande wa kulia.
Huenda hata baada ya watu fulani ambao tayari wamekwishashambuliwa na kiharusi sehemu hizo za mwili wakaendelea kutumia mikono na miguu yao kama vile wamepona, lakini muda si muda watagundua kwamba misuli yao hutetemeka sana kiasi kwamba miguu na mikono yao inaonekana kana kwamba kila mmoja unaelekea upande wake.
Dk. David Levine wa Kitovu cha Tiba cha Chuo Kikuu cha New York, Marekani, alikaririwa na jarida Psychology Today akisema kuwa waliokumbwa na ugonjwa huo "...wamepoteza aina ya hisia ambayo huwaambia ikiwa mkono au mguu wao unasonga au la na upo katika nafasi gani." Mgonjwa wa kiharusi anaweza kuuona mkono au mguu wake, lakini asiweze kuusogeza au kuuamrisha ufanye jambo fulani kama vile kubeba kijiko au hata kujifuta jasho.
Zaidi ya asilimia 15 ya watu waliopatwa na mshtuko wa akili hushambuliwa na magonjwa ya ghafla na nyakati nyingine kufuatiwa na vipindi vya kupoteza fahamu. Kuhisi maumivu huwa jambo la kawaida kwao.
Aliyekuwa kiongozi wa Urusi, Lenin, alifariki dunia kutokana na ugonjwa huo. Februari 3, 1924, Rais wa 28 wa Marekani, Woodrow Wilson, aliuawa kwa ugonjwa huo huo. Maneno yake ya mwisho yanayokumbukwa zaidi leo ni: "Mimi ni kipande kilichovunjika cha mashine--mimi kwisha." Aliharibiwa na kiharusi.
Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania akauawa kwa ugonjwa huo Oktoba 14, 1999, ingawa alikuwa na ugonjwa wa saratani ya damu ambayo nayo huenda ingesababisha kifo chake, lakini kiharusi kiliutangulia.
Baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu, Lenin aliwaambia wapambe wake hivi: "Kuna siku ambazo kitu hugusa miguu yangu na naamka kwa sababu inaonekana kama kwamba nashtushwa na umeme."
Kwa kushambuliwa na kiharusi, mambo mengi yanaweza kujitokeza. Wakati mwingine mhusika anaweza kupatwa na mambo ya kumvunjia heshima, kama vile mate kumtoka mdomoni. Wengine hupoteza kwa ghafla uwezo wao wa kuongea. Hii ni kama kutengwa kimawasiliano na jamaa, marafiki na familia yako.
Kama ilivyokuwa kwa Lenin, mwingine aliyepatwa na mshtuko wa akili aliliambia jarida Psychology Today hivi: "Kila wakati nilipokuwa nikijaribu kujieleza, hakuna (neno) lililotoka. Nililazimika kunyamaza kimya ...wala sikuweza kusoma. Maneno yalisikika kana kwamba watu walionizunguka walikuwa wakizungumza lugha ngeni ...Sikuweza kufahamu wala kutumia lugha."
Lakini si wagonjwa wote wa kiharusi wanaofikia hatua hiyo. Mgonjwa mwingine, Charles, alikaririwa na kitabu Brain Power cha Marilyn vos Savant & Leone Fleischer akisema: "Nilikuwa nikiyapanga maneno niliyotaka kusema, lakini yalitoka yakiwa yamevurugika na kupotoka..."
Katika kitabu Stroke: An Owner's Manual, Arthur Josephs anasema: "Misuli zaidi ya mia moja tofauti-tofauti huambatanishwa na kuongozwa na ubongo wakati wa kusema..." Ubongo unapoathiriwa na kiharusi hauwezi tena kuongoza misuli ya semi, kwa hiyo usemi huharibika.
Mambo mengi ya kukatisha tamaa katika eneo la usemi husababishwa na kiharusi. Kulingana na kitabu kilichotajwa hapo juu, huenda mtu asiyeweza kusema, akaweza kuimba. Mwingine anaweza kusema maneno kwa msukumo wa misuli hiyo tu lakini si wakati anapotaka kuyasema au anaweza kuzungumza bila kukoma.
Wengine hurudia-rudia maneno au fungu la maneno au kutumia maneno isivyofaa, wakisema ndiyo wanapomaanisha sivyo na kusema la wanapomaanisha ndiyo.
Wengine hujua maneno wanayotaka kuyatumia, lakini ubongo hauwezi kuuchochea mdomo kuyasema. Au wanaweza kugugumia maneno kwa sababu ya udhaifu wa misuli.
Madhara mengine ya kiharusi yanaweza kuwa ni kujeruhiwa kwa sehemu ya ubongo ambayo huongoza sauti. Matokeo yanaweza kuwa kwamba mazungumzo hayachangamshi.
Au kunaweza kuwa na ugumu wa kufahamu sauti za watu wengine. Vizuizi vya mawasiliano kama hivyo, pamoja na vilivyotajwa hapo juu, vinaweza kuwatenganisha washiriki wa familia na aliyeathirika, kama vile mume, mke na watoto.
Jarida Psychology Today lilimkariri mwanamume mmoja aliyewahi kuugua kiharusi akisema: "Kwa sababu huu (ugonjwa wa kiharusi) huathiri ishara za uso na mwili, utu wote mzima, kwa ghafla hakuna maelewano na wale uliowazoea awali ...Tulibadilikiana na mke wangu ...kwangu ilionekana kama vile nilikuwa na mke mpya kabisa, mtu niliyehitaji kumjua upya na kumzoea upya tena."
Kubadilika-badilika kwa hali kusikofaa, kuangua kilio au kicheko, kushikwa hasira kali ovyo, hisia za mashaka zisizo za kawaida, na huzuni nyingi kupita kiasi ni sehemu tu ya usumbufu na ya utu inayotia bumbuazi ambayo watu waliopatwa na kiharusi pamoja na familia zao huenda wakalazimika kukabiliana nayo.
Mmoja wa walioathiriwa na kiharusi, Gilbert, alitajwa na gazeti Drum la Afrika Kusini akisema: "Wakati mwingine (mimi) huwa mwenye hisia nyepesi, mambo madogo yananifanya ama nicheke au nilie ...ama nifurahi au nikasirike.
"Mara kwa mara ninapocheka, mtu anaweza kuuliza 'Mbona unacheka?' na kwa kweli siwezi kumwambia sababu ...Nahisi kama niko katika mwili mwingine, kana kwamba mimi ni mtu tofauti, si mtu yule niliyekuwa kabla ya kupata kiharusi."
Wakiishi na hali zinazodhoofisha akili na mwili, watu wengi hupatwa na mabadiliko ya hisia. Mjapan mmoja, Hiroyuki Nakaju, aliyepatwa na hitilafu ya kuongea na kupooza kwa sehemu baada ya kupatwa na kiharusi, aliliambia gazeti China Today hivi: "Hata kadiri muda unavyopita sikupata nafuu.
"Niking'amua kwamba nisingeweza kuendelea na hali yangu kama awali, nilikata tamaa ya maisha. Nilianza kulaumu vitu na watu ...nikahisi kwamba hisia zangu zitalipuka. Sikutenda tena kama mwanaume..."
Hali kama hizo huwakuta watu wengi tofauti kwa nyakati tofauti wakati wote wa kuugua kwao. Lakini matokeo ya kiharusi hayampati yule aliyeathirika peke yake. Si wagonjwa wa kiharusi tu ambao ni lazima wakabiliane na matokeo mabaya kabisa ya hali hiyo. Marafiki, jamaa na familia ya mhusika watashiriki pia.
Kwanza watakabiliana na hali ya kutambua kwamba mmoja wao ambaye wakati mmoja alikuwa na ufasaha na kujiweza, sasa anakuwa kinyume kabisa machoni pao, akifanya mambo kama mtoto mdogo kabisa anayelazimika kuwategemea wengine.
Uhusiano unaweza kuvurugika kwa kuwa huenda washiriki wa familia wakalazimika kuchukua madaraka ambayo hawayawezi au magumu kwao kuyahimili.
Mjapani mwingine, Haruko, aliliambia gazeti hilo hivi: "Mume wangu alipoteza kumbukumbuku la karibu kila jambo muhimu. Tulipoteza karibu kila kitu. "...Kilichonitaabisha zaidi ni kutoweza kuzungumza tena kwa uhuru niliokuwa nimeuzoea au kumwomba ushauri ...Ingawa tulijua kwamba wakati ungefika ambapo angefikia kiwango hiki, bado ni vigumu kwetu kukubali uhalisi wa hali yake..."
Elaine Fantle Shimberg katika kitabu Stroke: What Famililes Should Know, anaeleza kuwa "kumtunza mtu aliye na mshtuko wa akili--hata uwe unampenda kadiri gani--kunaweza kukuzidi nguvu. Misongo na madaraka hayapungui."
Katika matukio fulani matunzo ya hali ya juu yanayotolewa na wanaomhudumia yanaweza kudhuru afya na hisia. Hata hivyo, watunzaji au waangalizi wa watu waliokumbwa na kiharusi wanaweza kuathiriwa kisaikolojia kwa kipindi chote cha maisha yao.
Jambo gumu zaidi analokabiliana nalo mtunzaji ni mabadiliko ya tabia ya mhusika. Mwanasaikolojia Dk. Ronald Calvanio, aliwahi kusema: "Unapokuwa na ugonjwa unaoathiri kazi mbalimbali zinazotumia ubongo--jinsi mtu anavyofikiri, anavyoendesha maisha yake, na anavyokabiliana na hisia zake--kuna athari kubwa za kisaikolojia zinazotokoea kuliko jinsi inavyoweza kuwazika kwa urahisi na hubadili maisha ya familia kwa njia kubwa sana."
Mara nyingi, mabadiliko ya utu huenda yasionekane kwa wale ambao sio washiriki wa familia. Hivyo, watunzaji fulani hujihisi wakiwa wapweke na huibeba mizigo hiyo mizito wakiwa peke yao.
Ingawa hali ndivyo ilivyo, na kwa kuwa inaweza kumtokea mtu yeyote, je, inafaa kukata tamaa kana kwamba hakuna jambo lingine lolote lililobakia mara hali hiyo inapojitokeza?
Watu wengi waliopatwa na kiharusi pamoja na familia zao wamekabilianaje na mabadiliko katika maisha yao yanayosababishwa na kiharusi?
Akiwa amelazwa katika Hospitali ya Mount Meru, Arusha, mguu na mkono wake ukiwa umepooza, na ambaye tayari alikuwa ameshaanza kutumia baiskeli ya vilema, Husna Munissi (38), (sasa ni marehemu) alimuuliza daktari wake: "Je, kuna siku nitaweza tena kutumia mkono na mguu wangu?"
Husna alisikia jibu lenye matumaini: "Kadiri unavyofanya bidii, ndivyo utakavyoweza tena kutumia mkono na mguu wako, na ndivyo utakavyotimiza hilo haraka zaidi." Kwa kusikia jibu la faraja kadiri hiyo, alisema: "Niko tayari!"
Tiba pamoja na mtazamo mzuri kuelekea hali yake ulimsaidia aache kutumia baiskeli ya vilema, kisha kifaa cha kumsaidia kutembea, kisha bakora na hatimaye aliweza kurudi kazini.
Misaada mingi ya kuwezesha kuishi maisha ya kawaida baada ya kupatwa na kiharusi leo, huunga mkono ile dhana ya kwamba ikiwa sehemu moja ya ubongo imeharibika, maeneo mengine ya ubongo yanaweza kuchukua fungu la tishu zilizojeruhiwa.
Jarida Stroke linasema: "...Kusudi moja la tiba hiyo ni kuleta uwezekano wa maeneo hayo yaliyohusika na kuyachochea ili kuruhusu ubongo upange upya na kubadilika."
Hata hivyo, kupona kunategemea mambo mengine pia, kama vile mahali katika ubongo ambapo kiharusi kilitokea na ukubwa wa mshtuko huo wa akili, hali ya jumla ya afya ya mtu huyo, ubora wa utunzaji wa kitiba, na kutegemea wengine.
KIHARUSI au, kama wanasayansi wengine wanavyoutaja, 'mshtuko wa akili', ndiyo sababu kubwa ya vifo na ulemavu wa kudumu kwa watu katika nchi nyingi. Maneno yenyewe, yaani "mshtuko wa akili" (stroke--au kiharusi) yanaelezea hali ya ghafla ambayo "kushambuliwa kwa ubongo" hutokea.
Dakika moja, unaweza kujihisi vizuri, kitambo kidogo baadaye, unahisi kama vile umeshtuliwa na umeme au radi na kukuacha umelemaa--hivyo ndivyo kiharusi kinavyoweza kugeuza maisha yako kwa ghafla na kwa njia ya kushtua sana. Dakika moja unaweza kuwa mzima wa afya njema, dakika chache baadaye unagundua kuwa baadhi ya viungo vya mwili wako--mguu, mkono au mdomo--havifanyi kazi.
Ugonjwa huo ukiisha kukulemaza na kukudhoofisha kabisa, unaweza kukufanya ushindwe kuongea, ukiharibu kabisa hisia zako, ukibadili utu wako na uwezo wako wa kutambua mambo. Akili yako na uwezo wako wa kufikiri huharibika. Unaweza kushindwa kumtambua mkeo, mumeo, mwanao, nduguyo au mzazi uliyemzoea sana.
Kitabu All You Need To Know About Stroke kinasimulia kuhusu yaliyompata Alan Smith. Kinasema: "Siku ya Jumatano, alikuwa na umri wa miaka 54 akiwa katika hali yake ya kawaida na mwenye afya nzuri. Alhamisi (siku moja baadaye), alipokuwa na mkewe wakinunua vitu dukani, ghafla Smith alipoteza uwezo wake wa kuongea, na uso wake ukaumbuka. Mwili wake ulidhoofika, na alipepesuka, kama kwamba alikuwa amelewa." Kwanini? Kwa sababu "...Smith alikumbwa na kiharusi."
Baada ya kiharusi hicho, Smith alilemaa sana kiasi cha kushindwa kufanya mambo rahisi kufanywa--kama vile kuoga, kuvaa nguo na kula. Alishindwa kuandika, kusoma, kuchana nywele zake na kusalimiana na yeyote kwa kumpa mkono. Alikumbwa na vipindi vya kutokwa machozi ambayo hakutaka yatoke lakini hakuweza kuyazuia. Alikuwa akitokwa na mkojo asioweza kuuzuia pamoja na uchovu uliomzidi nguvu. Heshima yake ilivunjika.
Katika mambo yote hayo, uwezo wa kufikiri wa Smith haukuharibika, lakini wakati mwingine aliona aibu alipohisi kwamba labda wengine walimwona kama punguani. Ilimchukua muda mrefu kabla hajaweza kuongea tena, na alipoweza kufanya hivyo, alisema: "...Karibu nilihisi kwamba huo ulikuwa mwisho wa maisha yangu."
Kiharusi kinaweza kumpata mtu yeyote. Kitaalam, ubongo (wa mwanadamu) ndicho kiungo cha mwili kinachoweza kuharibika kwa urahisi sana, pengine kuliko kiungo kingine chochote, na huenda hicho ndicho kiungo cha maana zaidi kwa mwili wa mwanadamu kwa kuwa kinaongoza sehemu nyingine zote za mwili kikiagiza mkono, mguu, jicho au mdomo ufanye nini.
Kwa mujibu wa wanasayansi, ubongo wa binadamu, ukiwa na asilimia 2 tu ya uzani wote wa mwili wake, una chembe za neva zaidi ya bilioni kumi, ambazo huwasiliana daima ili kuzalisha fikra, mwendo na hisia.
Ubongo pia hutegemea hewa ya oksijeni. Ikiwa ubongo utanyimwa hewa hiyo, hata kama ni kwa sekunde chache tu, nyuroni zinazoweza kuharibika kwa urahisi hudhoofika haraka na kwa urahisi zaidi. Hilo likiendelea kwa zaidi ya dakika moja, madhara ya ubongo hutokea na kisha kuwa makubwa zaidi.
Hali hii huitwa ischemia, ukosefu wa oksijeni, hasa unaosababishwa na kuziba kwa arteri (moja ya mrija minene inayotoa damu kutoka moyoni na kupeleka sehemu nyingine za mwili). Ikiwa hali hiyo itaendelea kwa muda sekunde chache kiasi, matokeo ya mwisho yanakuwa ni mshtuko wa akili, au kiharusi (stroke).
Utaalam unaonyesha kuwa kila kiharusi ni tofauti na kinaweza kuwaathiri watu tofauti kwa njia tofauti. Ingawa hakuna yeyote anayepatwa na kila tokeo linalowezekana la kiharusi, matokeo yanaweza kutofautiana kuanzia madogo yasiyoonekana wazi hadi makubwa yanayoonekana wazi kwa njia ya maumivu. Sehemu ya ubongo inayopatwa na kiharusi huamua ni sehemu gani ya mwili itakayodhoofika.
Tatizo la kawaida linalosababishwa na kiharusi ni udhaifu wa kupooza miguu au mikono. Kwa kawaida, huo huwa ni upande mmoja tu wa mwili--upande ulio kinyume cha upande wa ubongo ambako kiharusi kimetokea.
Hivyo madhara ya ubongo wa upande wa kulia husababisha mwili kupooza upande wa kushoto, na madhara ya ubongo wa upande wa kushoto husababisha mwili kupooza upande wa kulia.
Huenda hata baada ya watu fulani ambao tayari wamekwishashambuliwa na kiharusi sehemu hizo za mwili wakaendelea kutumia mikono na miguu yao kama vile wamepona, lakini muda si muda watagundua kwamba misuli yao hutetemeka sana kiasi kwamba miguu na mikono yao inaonekana kana kwamba kila mmoja unaelekea upande wake.
Dk. David Levine wa Kitovu cha Tiba cha Chuo Kikuu cha New York, Marekani, alikaririwa na jarida Psychology Today akisema kuwa waliokumbwa na ugonjwa huo "...wamepoteza aina ya hisia ambayo huwaambia ikiwa mkono au mguu wao unasonga au la na upo katika nafasi gani." Mgonjwa wa kiharusi anaweza kuuona mkono au mguu wake, lakini asiweze kuusogeza au kuuamrisha ufanye jambo fulani kama vile kubeba kijiko au hata kujifuta jasho.
Zaidi ya asilimia 15 ya watu waliopatwa na mshtuko wa akili hushambuliwa na magonjwa ya ghafla na nyakati nyingine kufuatiwa na vipindi vya kupoteza fahamu. Kuhisi maumivu huwa jambo la kawaida kwao.
Aliyekuwa kiongozi wa Urusi, Lenin, alifariki dunia kutokana na ugonjwa huo. Februari 3, 1924, Rais wa 28 wa Marekani, Woodrow Wilson, aliuawa kwa ugonjwa huo huo. Maneno yake ya mwisho yanayokumbukwa zaidi leo ni: "Mimi ni kipande kilichovunjika cha mashine--mimi kwisha." Aliharibiwa na kiharusi.
Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania akauawa kwa ugonjwa huo Oktoba 14, 1999, ingawa alikuwa na ugonjwa wa saratani ya damu ambayo nayo huenda ingesababisha kifo chake, lakini kiharusi kiliutangulia.
Baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu, Lenin aliwaambia wapambe wake hivi: "Kuna siku ambazo kitu hugusa miguu yangu na naamka kwa sababu inaonekana kama kwamba nashtushwa na umeme."
Kwa kushambuliwa na kiharusi, mambo mengi yanaweza kujitokeza. Wakati mwingine mhusika anaweza kupatwa na mambo ya kumvunjia heshima, kama vile mate kumtoka mdomoni. Wengine hupoteza kwa ghafla uwezo wao wa kuongea. Hii ni kama kutengwa kimawasiliano na jamaa, marafiki na familia yako.
Kama ilivyokuwa kwa Lenin, mwingine aliyepatwa na mshtuko wa akili aliliambia jarida Psychology Today hivi: "Kila wakati nilipokuwa nikijaribu kujieleza, hakuna (neno) lililotoka. Nililazimika kunyamaza kimya ...wala sikuweza kusoma. Maneno yalisikika kana kwamba watu walionizunguka walikuwa wakizungumza lugha ngeni ...Sikuweza kufahamu wala kutumia lugha."
Lakini si wagonjwa wote wa kiharusi wanaofikia hatua hiyo. Mgonjwa mwingine, Charles, alikaririwa na kitabu Brain Power cha Marilyn vos Savant & Leone Fleischer akisema: "Nilikuwa nikiyapanga maneno niliyotaka kusema, lakini yalitoka yakiwa yamevurugika na kupotoka..."
Katika kitabu Stroke: An Owner's Manual, Arthur Josephs anasema: "Misuli zaidi ya mia moja tofauti-tofauti huambatanishwa na kuongozwa na ubongo wakati wa kusema..." Ubongo unapoathiriwa na kiharusi hauwezi tena kuongoza misuli ya semi, kwa hiyo usemi huharibika.
Mambo mengi ya kukatisha tamaa katika eneo la usemi husababishwa na kiharusi. Kulingana na kitabu kilichotajwa hapo juu, huenda mtu asiyeweza kusema, akaweza kuimba. Mwingine anaweza kusema maneno kwa msukumo wa misuli hiyo tu lakini si wakati anapotaka kuyasema au anaweza kuzungumza bila kukoma.
Wengine hurudia-rudia maneno au fungu la maneno au kutumia maneno isivyofaa, wakisema ndiyo wanapomaanisha sivyo na kusema la wanapomaanisha ndiyo.
Wengine hujua maneno wanayotaka kuyatumia, lakini ubongo hauwezi kuuchochea mdomo kuyasema. Au wanaweza kugugumia maneno kwa sababu ya udhaifu wa misuli.
Madhara mengine ya kiharusi yanaweza kuwa ni kujeruhiwa kwa sehemu ya ubongo ambayo huongoza sauti. Matokeo yanaweza kuwa kwamba mazungumzo hayachangamshi.
Au kunaweza kuwa na ugumu wa kufahamu sauti za watu wengine. Vizuizi vya mawasiliano kama hivyo, pamoja na vilivyotajwa hapo juu, vinaweza kuwatenganisha washiriki wa familia na aliyeathirika, kama vile mume, mke na watoto.
Jarida Psychology Today lilimkariri mwanamume mmoja aliyewahi kuugua kiharusi akisema: "Kwa sababu huu (ugonjwa wa kiharusi) huathiri ishara za uso na mwili, utu wote mzima, kwa ghafla hakuna maelewano na wale uliowazoea awali ...Tulibadilikiana na mke wangu ...kwangu ilionekana kama vile nilikuwa na mke mpya kabisa, mtu niliyehitaji kumjua upya na kumzoea upya tena."
Kubadilika-badilika kwa hali kusikofaa, kuangua kilio au kicheko, kushikwa hasira kali ovyo, hisia za mashaka zisizo za kawaida, na huzuni nyingi kupita kiasi ni sehemu tu ya usumbufu na ya utu inayotia bumbuazi ambayo watu waliopatwa na kiharusi pamoja na familia zao huenda wakalazimika kukabiliana nayo.
Mmoja wa walioathiriwa na kiharusi, Gilbert, alitajwa na gazeti Drum la Afrika Kusini akisema: "Wakati mwingine (mimi) huwa mwenye hisia nyepesi, mambo madogo yananifanya ama nicheke au nilie ...ama nifurahi au nikasirike.
"Mara kwa mara ninapocheka, mtu anaweza kuuliza 'Mbona unacheka?' na kwa kweli siwezi kumwambia sababu ...Nahisi kama niko katika mwili mwingine, kana kwamba mimi ni mtu tofauti, si mtu yule niliyekuwa kabla ya kupata kiharusi."
Wakiishi na hali zinazodhoofisha akili na mwili, watu wengi hupatwa na mabadiliko ya hisia. Mjapan mmoja, Hiroyuki Nakaju, aliyepatwa na hitilafu ya kuongea na kupooza kwa sehemu baada ya kupatwa na kiharusi, aliliambia gazeti China Today hivi: "Hata kadiri muda unavyopita sikupata nafuu.
"Niking'amua kwamba nisingeweza kuendelea na hali yangu kama awali, nilikata tamaa ya maisha. Nilianza kulaumu vitu na watu ...nikahisi kwamba hisia zangu zitalipuka. Sikutenda tena kama mwanaume..."
Hali kama hizo huwakuta watu wengi tofauti kwa nyakati tofauti wakati wote wa kuugua kwao. Lakini matokeo ya kiharusi hayampati yule aliyeathirika peke yake. Si wagonjwa wa kiharusi tu ambao ni lazima wakabiliane na matokeo mabaya kabisa ya hali hiyo. Marafiki, jamaa na familia ya mhusika watashiriki pia.
Kwanza watakabiliana na hali ya kutambua kwamba mmoja wao ambaye wakati mmoja alikuwa na ufasaha na kujiweza, sasa anakuwa kinyume kabisa machoni pao, akifanya mambo kama mtoto mdogo kabisa anayelazimika kuwategemea wengine.
Uhusiano unaweza kuvurugika kwa kuwa huenda washiriki wa familia wakalazimika kuchukua madaraka ambayo hawayawezi au magumu kwao kuyahimili.
Mjapani mwingine, Haruko, aliliambia gazeti hilo hivi: "Mume wangu alipoteza kumbukumbuku la karibu kila jambo muhimu. Tulipoteza karibu kila kitu. "...Kilichonitaabisha zaidi ni kutoweza kuzungumza tena kwa uhuru niliokuwa nimeuzoea au kumwomba ushauri ...Ingawa tulijua kwamba wakati ungefika ambapo angefikia kiwango hiki, bado ni vigumu kwetu kukubali uhalisi wa hali yake..."
Elaine Fantle Shimberg katika kitabu Stroke: What Famililes Should Know, anaeleza kuwa "kumtunza mtu aliye na mshtuko wa akili--hata uwe unampenda kadiri gani--kunaweza kukuzidi nguvu. Misongo na madaraka hayapungui."
Katika matukio fulani matunzo ya hali ya juu yanayotolewa na wanaomhudumia yanaweza kudhuru afya na hisia. Hata hivyo, watunzaji au waangalizi wa watu waliokumbwa na kiharusi wanaweza kuathiriwa kisaikolojia kwa kipindi chote cha maisha yao.
Jambo gumu zaidi analokabiliana nalo mtunzaji ni mabadiliko ya tabia ya mhusika. Mwanasaikolojia Dk. Ronald Calvanio, aliwahi kusema: "Unapokuwa na ugonjwa unaoathiri kazi mbalimbali zinazotumia ubongo--jinsi mtu anavyofikiri, anavyoendesha maisha yake, na anavyokabiliana na hisia zake--kuna athari kubwa za kisaikolojia zinazotokoea kuliko jinsi inavyoweza kuwazika kwa urahisi na hubadili maisha ya familia kwa njia kubwa sana."
Mara nyingi, mabadiliko ya utu huenda yasionekane kwa wale ambao sio washiriki wa familia. Hivyo, watunzaji fulani hujihisi wakiwa wapweke na huibeba mizigo hiyo mizito wakiwa peke yao.
Ingawa hali ndivyo ilivyo, na kwa kuwa inaweza kumtokea mtu yeyote, je, inafaa kukata tamaa kana kwamba hakuna jambo lingine lolote lililobakia mara hali hiyo inapojitokeza?
Watu wengi waliopatwa na kiharusi pamoja na familia zao wamekabilianaje na mabadiliko katika maisha yao yanayosababishwa na kiharusi?
Akiwa amelazwa katika Hospitali ya Mount Meru, Arusha, mguu na mkono wake ukiwa umepooza, na ambaye tayari alikuwa ameshaanza kutumia baiskeli ya vilema, Husna Munissi (38), (sasa ni marehemu) alimuuliza daktari wake: "Je, kuna siku nitaweza tena kutumia mkono na mguu wangu?"
Husna alisikia jibu lenye matumaini: "Kadiri unavyofanya bidii, ndivyo utakavyoweza tena kutumia mkono na mguu wako, na ndivyo utakavyotimiza hilo haraka zaidi." Kwa kusikia jibu la faraja kadiri hiyo, alisema: "Niko tayari!"
Tiba pamoja na mtazamo mzuri kuelekea hali yake ulimsaidia aache kutumia baiskeli ya vilema, kisha kifaa cha kumsaidia kutembea, kisha bakora na hatimaye aliweza kurudi kazini.
Misaada mingi ya kuwezesha kuishi maisha ya kawaida baada ya kupatwa na kiharusi leo, huunga mkono ile dhana ya kwamba ikiwa sehemu moja ya ubongo imeharibika, maeneo mengine ya ubongo yanaweza kuchukua fungu la tishu zilizojeruhiwa.
Jarida Stroke linasema: "...Kusudi moja la tiba hiyo ni kuleta uwezekano wa maeneo hayo yaliyohusika na kuyachochea ili kuruhusu ubongo upange upya na kubadilika."
Hata hivyo, kupona kunategemea mambo mengine pia, kama vile mahali katika ubongo ambapo kiharusi kilitokea na ukubwa wa mshtuko huo wa akili, hali ya jumla ya afya ya mtu huyo, ubora wa utunzaji wa kitiba, na kutegemea wengine.