|
Post by Yona Maro on Dec 12, 2005 3:21:38 GMT -5
Mchungaji wa kweli aliyeitwa na Mungu kwa ajili ya utumishi wake hawezi kupata ukimwi kwa sababu hali na tamaa ya kutenda dhambi ndani yake imetoweshwa kwa kule kumwamini na Kumpokea Yesu awe Bwana na mwokozi wa maisha yake.Kwa hali hiyo mimi naamini waliopata ukimwi ni WACHUNGAJI WA MISHAHARA AMBAO HAWAJAOKOKA NA WAMEWEKWA KWENYE UCHUNGAJI NA VIONGOZI WA DINI ZAO NA SIO MUNGU ALIYE MTAKATIFU. Na pengine wachungaji hao waliingia utumishi huo kwa tamaa zao wenyewe na sio wito. Kwa wachungaji wa jinsi hii ni hatari, ni bora wakafuata ushauri nasaha na wakajilinda kama wanaharakati wa Ukimwi wanavyoshauri kwa kuwa na mpenzi mmoja akishindwa avae kondomu , vinginevyo atakufa na atahukumiwa kwa dhambi hiyo mbaya na huku akijifanya ni mtumishi wa Mungu.
from nipashe
|
|