Post by Yona Maro on Dec 12, 2005 3:14:25 GMT -5
KIPINDI ambacho kilikuwa kinangojewa kwa hamu, kipindi cha uchaguzi, sasa kimefika.
NI kipindi ambacho Watanzania watakitumia kwa ajili ya kuchagua viongozi wao wa serikali ya awamu ya nne nchini.
BAADA ya malumbano ya kisiasa ya muda mrefu, kwenye kampeni, ni wazi kuwa Watanzania wanajua nini wanachotakiwa kukifanya siku ya upigaji kura.
TUNAPENDA kuwakumbusha Watanzania kwa ujumla haja ya kujiandaa na siri ya moyoni na kwenda kuiweka katika karatasi kwani kura yako ni muhimu sana katika kufanikisha maendeleo ya nchi, amani na utulivu.
KUTOKANA na hilo ni wazi kwamba wapiga kura ni lazima wafike katika vituo vyao wakiwa na vitambulisho vyao, kujiweka katika foleni na kumchagua Rais, mbunge na diwani kwa utulivu.
PIA wapiga kura hawana sababu ya kuogopa kwenda kwenye zoezi hilo kwa kuwa ni wajibu wao na ni wajibu wa dola kuwalinda watu wake, pasishaka Mungu atatubarikli na kutuvusha salama kama tutamuomba kwa dhati na kwa matumaini makubwa.
WALE labda wanaofikiria kufanya fujo, Mungu na apishe mbali, tunaomba wabadilike kwani ufanisi wa zoezi zima kunategemea mno ukweli wa ndani ya utulivu unaostahili kuwepo.
KUTOKANA na utulivu ambao unatakiwa kufuatwa na kila mmoja hakuna haja ya kuogopa kwenda katika vituo vya kupiga kura, kufanya zoezi hilo na kurejea nyumbani kusubiri matokeo.
NI vyema tukawa na subira yenye heri tupu na tukaacha jazba siku ya kupiga kura, kila mtu akiheshimu utaratibu uliowekwa na wale wenye dhamana kuhakikisha kwamba wanaitekeleza dhamana hiyo.
KWA kufuata maagizo ya Tume tutaweza kabisa kutengeneza mazingira mazuri ya amani na hivyo kuwezesha kufanyika kwa zoezi lenyewe kwa haki na uhuru kabisa.
KWA wale wanaoitakia mema Tanzania kipindi cha kuelekea siku ya kura ni wajibu wao kukumbusha amani na huenda ikawa ni sahihi kwa watu kuiombea nchi hii kwa Mungu ili aweze kuivusha salama katika hatua yake hii muhimu.
TUNAHITAJI sana baraka za Mungu katika kufanikisha zoezi hili, ili kila mmoja awe na subira katika nafsi yake katika kufanikisha uchaguzi wa viongozi ambao watatuweka pamoja na kutuwezesha kuendelea na shughuli zetu kwa amani.
NA tunamalizia wito wetu kwa kutaka kila mmoja katika nafasi yake kuhakikisha amani ya zoezi, kuacha mitafaruku ya kipuuzi ambayo inachochea hasira na hivyo busara kutawala katika kuchagua mkuu wa nchi na wale wanaotusaidia katika kutunga sheria na kufuatilia ufanisi wa serikali,MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRIKA.
SOURCE: Nipashe
NI kipindi ambacho Watanzania watakitumia kwa ajili ya kuchagua viongozi wao wa serikali ya awamu ya nne nchini.
BAADA ya malumbano ya kisiasa ya muda mrefu, kwenye kampeni, ni wazi kuwa Watanzania wanajua nini wanachotakiwa kukifanya siku ya upigaji kura.
TUNAPENDA kuwakumbusha Watanzania kwa ujumla haja ya kujiandaa na siri ya moyoni na kwenda kuiweka katika karatasi kwani kura yako ni muhimu sana katika kufanikisha maendeleo ya nchi, amani na utulivu.
KUTOKANA na hilo ni wazi kwamba wapiga kura ni lazima wafike katika vituo vyao wakiwa na vitambulisho vyao, kujiweka katika foleni na kumchagua Rais, mbunge na diwani kwa utulivu.
PIA wapiga kura hawana sababu ya kuogopa kwenda kwenye zoezi hilo kwa kuwa ni wajibu wao na ni wajibu wa dola kuwalinda watu wake, pasishaka Mungu atatubarikli na kutuvusha salama kama tutamuomba kwa dhati na kwa matumaini makubwa.
WALE labda wanaofikiria kufanya fujo, Mungu na apishe mbali, tunaomba wabadilike kwani ufanisi wa zoezi zima kunategemea mno ukweli wa ndani ya utulivu unaostahili kuwepo.
KUTOKANA na utulivu ambao unatakiwa kufuatwa na kila mmoja hakuna haja ya kuogopa kwenda katika vituo vya kupiga kura, kufanya zoezi hilo na kurejea nyumbani kusubiri matokeo.
NI vyema tukawa na subira yenye heri tupu na tukaacha jazba siku ya kupiga kura, kila mtu akiheshimu utaratibu uliowekwa na wale wenye dhamana kuhakikisha kwamba wanaitekeleza dhamana hiyo.
KWA kufuata maagizo ya Tume tutaweza kabisa kutengeneza mazingira mazuri ya amani na hivyo kuwezesha kufanyika kwa zoezi lenyewe kwa haki na uhuru kabisa.
KWA wale wanaoitakia mema Tanzania kipindi cha kuelekea siku ya kura ni wajibu wao kukumbusha amani na huenda ikawa ni sahihi kwa watu kuiombea nchi hii kwa Mungu ili aweze kuivusha salama katika hatua yake hii muhimu.
TUNAHITAJI sana baraka za Mungu katika kufanikisha zoezi hili, ili kila mmoja awe na subira katika nafsi yake katika kufanikisha uchaguzi wa viongozi ambao watatuweka pamoja na kutuwezesha kuendelea na shughuli zetu kwa amani.
NA tunamalizia wito wetu kwa kutaka kila mmoja katika nafasi yake kuhakikisha amani ya zoezi, kuacha mitafaruku ya kipuuzi ambayo inachochea hasira na hivyo busara kutawala katika kuchagua mkuu wa nchi na wale wanaotusaidia katika kutunga sheria na kufuatilia ufanisi wa serikali,MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRIKA.
SOURCE: Nipashe